Thursday, July 12, 2012


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Meya wa  Manispaa ya Ilala Mhe.Jerry Silaa wakati Meya huyo alipomtembelea na kufanya naye mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya Manispaa hiyo. Kiutawala Meya wa Manispaa ya Ilala,ana umuhimu wa aina yake hususani tukizingatia kwamba Ikulu(makazi rasmi ya Rais nchini Tanzania) yapo katika Wilaya ya Ilala. Meya Jerry Slaa,alitumia wakati huo kumkabidhi Rais Kikwete baadhi ya nyaraka muhimu(kama zinavyoonekana mikononi mwa Meya) kuhusiana na masuala hayo hayo ya maendeleo katika Manispaa ya Ilala.
(picha na Freddy Maro)

MAMLAKA YA ELIMU YAPONGEZA TAMASHA LA MATUMAINI

Esther Bayo akizungumza na wanahabari  (hawapo pichani).
Meneja Habari, Elimu na Mawasiliano wa mamlaka hiyo, Sylvia Gunza,  akifafanua jambo kwenye mkutano huo.

Mishemishe za mkutano huo zikiendelea.…

MREMBO BORA WA MISS SINZA 2012 KUPATIKANA KESHO, TWANGA KUWASHA MOTO

 Mwalimu wa warembo wa shindano la kumsaka Miss Sinza 2012, Mwajabu Juma, akitoa maelekezo kwa warembo hao wakati wa mazoezi yao ya mwisho kujiandaa na shindano hilo litakalofanyika kesho katika Ukumbi wa Mawela Social, karibu na Vatcan Hoteli, Sinza. Shindano hilo litasindikizwa na burudani kabambe na shoo ya kufa mtu kutoka kwa Bendi ya African Stars, watakaokuwa wakitambulisha pia baadhi ya nyimbo zao mpya kwa mara ya kwanza, pamoja na msanii wa Vichekesho kutoka kundi la Ze Commedy linalorusha michezo yake kupitia Televisheni ya Chanel 5, Masawe Mtata, ambaye pia atakuwa akitambulisha video ya wimbo wake mpya uitwao Uongo Kweli.…

BABA DIAMOND...



Na George Kayala na Haruni Sanchawa
BABA mzazi wa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’, (pichani) Abdul Juma ameibuka ambapo mbali na tukio hilo pia amenena mambo mazito kuhusu mwanaye huyo huku akimsukumia tuhuma nzito mama mtu, Amani linaanika kila kitu.

ASAKWA PANDE ZOTE ZA DAR

Awali lilitangulia zoezi la kumsaka baba Diamond katika…

AUNT ANA MIMBA MIEZI SITA



Na Shakoor Jongo
SIKU chache baada ya staa wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel kuripotiwa kufunga ndoa mjini Dubai, mchumba wa staa huyo aliyetambulika kwa jina moja tu la Jeff amesema kuwa, anashangazwa na Aunt kuolewa huku akiwa na ujauzito wake, Amani linashuka na mistari ya habari hii.
Akizungumza na Amani jijini Dar hivi karibuni, Jeff amesema kuwa taarifa za kuolewa kwa Aunt alizipata akiwa nchini China na kushtuka sana.
“Kinachonishangza ni huyo jamaa anafungaje ndoa na mwanamke ambaye ana ujauzito wangu wa miezi sita ambao aliondoka nao kwenda Dubai?” alihoji Jeff.
Jeff aliendelea…

BARNABA ANASWA...

Posted by GLOBAL on July 12, 2012 at 8:50am 9 Comments


Stori na Mwandishi weu Zanzibar
Siku chache baada ya mwanamuziki Barnaba Elias kutangaza kujaaliwa mtoto wa kiume aliyezaa na mwanamke anayeishi naye, msanii huyo hivi karibuni alinaswa akiwa na demu mwingine kwenye nyumba ya kulala wageni mjini hapa.
Barnaba alifika Zanzibar kwa ajili ya kufanya shoo kwenye Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) linaloendelea Kisiwani Unguja ambapo paparazi wetu akiwa kwenye gesti ya Malindi alimuona binti mmoja akiingia na kumtaka mhudumu ampe funguo za chumba alicholala msanii huyo.
“Mimi naomba unipe…

TAARIFA KUTOKA TFF LEO

SIMBA, WAGANDA SASA KUCHEZA JUMAPILI
Mechi ya Simba na URA ya Uganda kuwania Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) iliyokuwa ichezwe Jumatatu (Julai 16 mwaka huu) sasa itafanyika Jumapili (Julai 15 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limefanya mabadiliko hayo kutokana na fainali ya Copa Coca-Cola 2012 iliyokuwa ichezwe kwenye uwanja huo kuhamishiwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.
Kutokana na mabadiliko hayo, mbali ya mechi ya Simba na URA itakayoanza saa 10 kamili jioni, mechi nyingine Jumapili itakuwa kati ya Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) dhidi ya Ports ya…

Vodacom Internet users get up to FIVE times more access

 Vodacom subscribers have another reason to smile as Vodacom enhances its Wajanja Internet bundles offering customers up to five times more internet access!
Prepaid Subscribers will also surf Wikipedia, Facebook and Twitter for FREE every day enabling them to learn more, get ahead and stay connected to their social networks.
"Students are now making use of the internet for reference and research on various subjects. It is therefore important to offer Wikipedia for free to give them access to important information that will assist with their studies. The youth form a large chunk of our customers and we hope with the free Wikipedia will benefit them immensely,” said Rene Meza, Vodacom Tanzania Managing Director, explaining that the new volumes aim at giving the best customer experience for data users.
“For as…


MATUKIO MBALIMBALI YA ZIARA YA RAIS KIKWETE NCHINI UINGEREZA


 Rais Jakaya Mrisho kikwete, Rais Yoweri Kaguta Museveni wa Uganda na mkewe Mama Janet Museveni, Waziri Mdogo wa Uingereza wa Maendeleo ya Kimataifa Bw. Stephen O'Brien (kulia) na Mama Melinda Gates wakibadilishana mawazo kabla ya kuhutubia katika mkutano wa kimataifa wa viongozi kujadili Uzazi wa Mpango kwa nchi masikini zaidi duniani katika ukumbi wa Queen Elizabeth II jijini London July 11, 2012. Mkutano huo ni wa kwanza wa aina yake duniani na umeanzisha Mchakato wa Dunia ambao utalenga kuwawezesha wanawake wapatao milioni 120 katika nchi masikini zaidi duniani kupata habari, huduma na mahitaji ya kupanga uzazi bora zaidi na kuokoa…

No comments:

Post a Comment