Thursday, July 12, 2012



Mratibu Mkazi wa Umoja Mataifa nchini Dr. Alberic Kacou (katikati) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere kumpokea Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr. Asha Rose Migiro aliyemaliza muda wake leo wakati akirejea nchini Tanzania. Kushoto ni Afisa wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa nchini Hoyce Temu.

Baadhi ya Mabalozi, Wahadhiri na Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa wamejipanga kumpokea Dr. Asha Rose Migiro.

Msafara wa Dr. Asha Rose Migiro ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Mh. Benard Membe (gari la pili) kuelekea sehemu maalum ya mapokezi.

Dr. Asha Rose Migiro akishuka kwenye gari yake baada ya kukanyaga Ardhi ya Tanzania.


 
  • Kenyan Rapper-Singer-Songwriter Breaks New Ground With Historic Deal

Sony Music Entertainment Africa is proud to announce the signing of rising African rapper, Xtatic, to a multi-album and full management deal.

The deal marks a first for a Kenyan artist and sees the hotshot rapper, songwriter and performer (born Gloria Edna Mecheo) join a global roster of artists on Sony’s RCA label that includes the likes of Usher, Chris Brown, R Kelly and Pink.

The 21-year-old was recently in Johannesburg, recording tracks for her debut full-length album with hot new producers ‘The Fahrenheitz’. The record will be released later in 2012 as part of the multi-album recording deal Xtatic has inked with Sony and is being preceded by the first single, ‘WILD!’ due to hit the airways in the next two weeks. Xtatic has also signed a full services management deal with Sony Music and ROCKSTAR4000, and worldwide Music Publishing deal with ROCKSTAR PUBLISHING, positioning her for a full assault on the South African, Nigerian, Kenyan, Pan African and, ultimately, global music scenes.

“We’re convinced that Xtatic has the kind of standout talent that will take her into many different markets and are thrilled to welcome her into the Sony recording family,” says RCA Africa Director, Spiro Damaskinos.


Napenda kuwatangazia wana-Bumbuli kwamba ile ahadi niliyotoa wakati wa kampeni – ahadi ya kuanzisha Shirika la Maendeleo Bumbuli – imetimia.  Shirika limepata usajili, limefungua ofisi, lina watumishi wa mwanzo na tayari ipo miradi minne ambayo utekelezaji wake utaanza mara moja. Tutazindua Shirika hili tarehe 4 Agosti 2012, katika mkutano wangu na wana-Bumbuli waishio Dar es Salaam na mikoa ya jirani, na baadaye katika mikutano na wananchi jimboni Bumbuli.

Chimbuko

Nilipoamua kugombea Ubunge wa Bumbuli mwaka 2010, niliamua kwamba katika utumishi wangu kama Mbunge nitashirikiana na Wana-Bumbuli pamoja na marafiki na washirika wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi katika kuleta mageuzi ya kiuchumi na kijamii Bumbuli. Jimbo letu ni kati ya majimbo yaliyo nyuma kimaendeleo kwa kiasi kikubwa na hivyo kuhitaji jitihada za ziada – zaidi ya zile za Serikali. Katika kufikia lengo hilo, niliahidi kuanzisha Shirika litakaloratibu shughuli za maendeleo katika Jimbo.
Nilifikia uamuzi wa kuanzisha Shirika nikitambua kwa dhati uwepo wa  jitihada nzuri za serikali katika kuboresha maisha ya watu wa Bumbuli nikitegemea pia serikali kuendeleza jitihada zaidi. Hata hivyo natambua kwamba kazi ya maendeleo si kazi ya serikali pekee, inahitaji ushiriki wa kila mmoja na hasa sekta binafsi ili kuisadia juhudi za serikali kufikia malengo ya maendeleo. Nilitaka kuchambua uwezo wa watu binafsi, wafanyabiashara na taasisi mbalimbali katika kupanua wigo wa ajira na shughuli za kipato kwa watu wa Bumbuli kupitia uwekezaji katika jamii.

No comments:

Post a Comment